Saturday, August 16, 2014

Namna ya kumtoa jini katika mwili wa mwanadamu.

Kila Tiba kati ya zifuatazo ni yenye kujitegemea.Chagua iliyo rahisi kwako.Isipokufaa ndipo uchague nyengine.


Sharti za tabibu
1.Anatakiwa awe anaswali swala tano kila siku.2.Aache kumshirikisha Mwenyezi Mungu.3Asiwe mchawi.4.Awe anafunga suna siku za Jumatatu na Alkhamis pamoja na masiku meupe.5.Awe anapenda kusimama usiku katika ibada ya swala za usiku kama tahajjud.6.Awe anafanya uradi kila siku na kuleta dua za kumuomba Mwenyezi Mungu ampe nguvu za kupambana na majini.

Namna ya kumtoa jini katika mwili wa mwanadamu.

Kwanza tabibu atie udhu na kisha aombe dua zifuatazo na baadae kumswalia Mtume mara mia moja wakati huo mgonjwa awe amekaa chini.
Dua ya 1:Ayatul Qursiy mara 7.
Dua ya 2:Surat Dhaariyaat mara 3
Dua ya 3:Surat Ikhlaswi mara 3
Dua ya 4:Suratin Nnaas mara 3
Dua ya 5:Soma HASBUNA LLAAH WA NEEMAL WAKEELmara 100 na kumalizia na Laa Haula wala Quwwata illa Bilaahil Adhwiim.
Utaratibu huu utarudiwa kila siku kwa muda wa wiki 1.

ZITAMBUE NDOTO ZAKO UZIOTAZO



NDOTO
(1) Ukiota  unacheza karata= utapata bahati
(2) Ukiota  uakula kabeji= utapata maradhi ya kujitakia.
(3) Ukiota  unaona karanga= vulugu haziishi nyumbani.
(4) Ukiota  umevaa nguo mpya= utazawadiwa
(5) Ukiota  umevaa nguo nyeusi= utapata mikosi.
(6) Ukiota  umevua nguo= utapata hasala lakini kama nguohiyo ni cchafu= mikosi ita kuondoka.
(7) Ukiota vaa nguo zilizo chanika= utapatwa na aibu.
(8) Ukiota umevaa nguo za mapambo au za maua= utapata furaha.
(9) Ukiota unaendesha kigari cha farasi= utakua ombaomba.
(10) Ukiota unachoma mkaa= utaoa mwanamke alie achika.
(11) Ukiota umepata mafua= una maadui wa kisilisili.
(12) Ukiota umeona mahindi= utapata faida katika shugurizako.
(13) Ukiota uko kwenye ukumbi wa mziki = utapata habari nzuli toka kwa rafikiyako wa karibu.
(14) Ukiota kiza kinene= utadanganywa au utatapeliwa.
(15) Ukiota unaona giza kasha ukawa mwanga= kama ni mfungwa atafunguliwa na kama si mfungwa ni dalili ya mamboyako kifunguka.
(16) Ukiota uko msibani= harusi. Ila ndotohii ikijirudia ni dalili ya jinni maiti.
(17) Ukiota jinni limekudhulu au umeliogopa kupita kiasi= kuna hatali mbeleni.
(18) Ukiota unchimba shimo na kasha likapotea= nidalili ya kuikosa mazao na utafukuzwakazi na pia ni dalili ya kukosa nvua.
(19) Ukiota unatumbukia shimoni= utapata mikosi na utatesekasana ki maisha.
(20) Ukiota unavuka mto kwa kutumia gogo= utapata watetezi katika mamboyako na kama unakesi utasshinda kwa msaada wa mtu.
(21) Ukiota umemuona dragon= utapata utajili kwa njia ya mazingali(madawa)
(22) Ukiota umemuona chatu= utapata utajili.
(23) Mwanaume akiota anaona nguo ya kike imeanikwa= atapatwa na mabalaa.
(24) Ukiota unakunywamaji wakati jia linachomoza na una kinywa kwa kutumia mkono wa kushoto= utapata maradhi.
(25) Ukiota ulewa pombe kupita kiasi= utapata marafiki wa maana na pia ni mafanikio ki mapenzi.
(26) Ukiota unazama ndani ya maji =nidalili ya kupata mikosi.
(27) Ukiota unamuona mtu anazama ndani ya maji= mikosiyako itaisha.
(28) Ukiota unonafunza= kaachonjo kuna maadui.
(29) Ukiota unakula= mikosi.
(30) Ukiota unalishwakitu= nikweli umelishwa.
(31) Ukiota umekufa kwa kupiganiadini= amalizako ni njema.
(32) Ukiota unakunywa maziwa= utapata mafanikio.
(33) Ukiota mkeo matiti ni makubwa= utapata mafanikio.
(34) Ukiota mbalamwezi inang”aa= utapata furaha na mafanikio
(35) Ukiota umepotezapesa= utapata hasala ki biashara.
(36) Ukiota umepatahela = mafanikio ila si kuokota.
(37) Ukiota unaokotahela= utapata mikosi.
(38) Ukiota umekunja chuma= umewashinda maadui.
(39) Ukiota nyota inang”aa wakatihuo una mchumba= mtafarakana na mchumbawako.
(40) Ukiota nyota imeanguka= afyanjema.
(41) Ukiota umemuona bata mzinga= ndoayenu ni ya mafanikio na mtapata watotowengi.
(42) Ukiota unang”okajino= utapoteza rafiki wa karibu.
(43) Ukiota umeng”oka meno ya mbele utapoteza marafiki wengi na ndugu watakuchukuya.
(44) Ukiota unikunywa maji masafi= utapata furaha.
(45) Ukiota unakunywa maji machafu= matatizo yanakunyemeleya.
(46) Ukiota unaona maba= utapata maumivu.
(47) Ukiota unachomwa mwiba= utapoteza pesa.
(48) Ukiota radi inapiga= mafanikio katika biashara.
(49) Ukiota radi imekupiga= umekumbwa na jinni.
(50) Ukiota umemuona kobu= biashara zako zitaenda polepole
(51)             ukiota unakulakobe= mtalekebisha tofautizenu za ndoa.
(52) Mwanamke alie achika akiota anafunga ndoa= ni nikosi.
(53) Mgonjwa akiota anafungandoa na mwanamke alie achika= atakufa.
(54) Ukiota unalia= ni fulaha na upendo.
(55) Mgonjwa akiota anafunga ndoa na msichana ambae haja olewa= atapona,
(56) Ukiota unaona karatasi nyeupe= utapata mke wa maana na watoto wa heli.
(57) Ukiota unachana karatasi= utaendekeza umalaya.
(58) Ukiota unatembea katika bara bara lililo nyooka= mafanikio mbeleyako na ni afya njema.
(59) Manamme akiota anamuona tausi= atapata mke mzuri na atatajilika.
(60) Mwanamke akiota anamuona tausi atapata mwanamme tajiri lakini ni muongo muongo.
(61) Ukiota unamuona bundi= nimikosi na vifungo
(62) Ukiota njegele zimepikwa= mafanikio.
(63) Ukiota unakula mkaa= utapata mikosi.
(64) Ukiota unaona vitunguu= utapata habali njema.
(65) Mwanamme akiota anaona vitunguu= atapata mwanamke mwaminifu ila ni mwenye hasira.
(66) Ukiota unachimba kaburi= jinni maiti na pia ni dalili yakwa mba kuna tabia unayoifanya si nzuli itkuingiza katika wakati mgumu.
(67) Ukiota  unalima na ng”ombe= mafanikio.
(68) Ukiota watu wanalima na ng”ombe lakini zinazama= nidalili ya mavuno mabaya.
(69) Ukiota watu wanalima juu yam lima= utapoteza mifugo.
(70) Ukiota umepewa tundadam chachu= utagombana na rafikiyako.
(71) Tajila akiota nasali= furaha
(72) Maskini akiota anasali= matatizo na mikosi.
(73) Mwanamme akiota anachota maji kisimani= ataoa.
(74) Mwanamke akiota anachota maji kisimani= ataolewa.
(75) Ukiota una kunywa wiski= ni mikosi, mabalaa, majuto.
(76) Ukiota upepo wa kimbunga= utaoa mke mwenye makelele.
(77) Tajili akiota amebemba mbao= mikosi
(78) Maskini akiota amebeba mbao= bahati.
(79) Ukiota una andika=jihadharili na kaulizako.
(80) Ukiota unapiga miayo= rafikizako wamekuchoka.
(81) Ukiota unaona kitu chochote cha njano= mafalakano katika mapenzi yenu.
(82) Ukiota unamuona punda milia= kua mwangalifu katika maishayako.
(83) Ukiota watu wanapiga talumbeta.= utapata mikosi na matatizo.
(84) Ukiota unaona ndim= utapata ugonvi au kutukanwa.
(85) Ukiota unaona mwanamke bikra= utapata habali njema.
(86) Maskini akiota anatapika  atapatapesa lakini kwa tajili atafilisika.
(87) Ukiota vita= matatizo na huzuni.
(88) Ukiota unamuona mamamkwe= utaugua.
(89) Ukiota unaongeana mama yako vizuli= uta fanikiwa kwa lolote.
(90) Ukiota mpishi yuko ndani ya nyumba= utao mwanamke wa maana na kama una matatizo. Yataondoka.
(91) Mgonjwa akiota anamuona mpishi= haliyake itakua mbaya.
(92) Ukiota unaona kisu= mafaninio.
(93) Ukiota unamuona paka utaibiwa.
(94) Ukiota paka amekuuma= utaletewa habali za uongo.
(95) Ukiota unakula keki= furaha na mafanikio.
(96) Ukiota mshumaa unawake kasha ukazimika= mamboyako yatahalibika pia ni ishala ya kufilisika.
(97) Mgonjwa akiota mshumaa umawashwa = atapona.
(98) Ukiota mshumaa ambao haujawashwa= utapata zawadi nono.
(99) Ukiota unaona watoto wengi ndane ya nyumba=  nadalili ya kufungika kwa kizazi
(100)             Ukiota unakunywa kahawa= marafikizako ndo maaduizako.

NDOTO ZISIZO TAFSILIKA

52.NDOTO ZISIZOFASIRIWA.

Kuna baadhi ya ndoto huwa haziwezekani kufasiriwa kutokana na jinsi hali ya mtu wakati alipoota au kufuatana na ndoto jinsi ilivyootwa. Nazo ni kama zifuatazo:

1. Wakati mtu kalala hali ana janaba.
2. Wakati mtu kalala hali kalewa.
3. Mtu kabla ya kulala akawa anafikiri kitu na kukitamani kitu kile kisha akaota vilevile.
4. Ndoto mbaya yenye kukhofisha na kuhuzunisha ya kutokana na Shetani.

121.FAIDA ZA NDOTO.
Baada ya utafiti katika kujua ndoto nimekuja kufahamu kwamba Mwenyezi Mungu S.W.T. ametukirimu sisi binadamu na hasa Waislamu wema kwa kuota ndoto za kweli kwa kuwabashiria ambazo ndoto hizo zina faida kama ifuatavyo:

1. Ni njia mojawapo ya kuwaona na kujua hali za maiti ambao khabari zao zimetukatikia walipoihama dunia. Kama alivyotuhadithia Sahaba Ibn Abbas R.A.A. kwamba roho za wale watu waliokufa zinakutana na roho za walio hai na kuulizana baina yao. Pia huenda tukafahamu hali ya yule maiti ima katika raha au taabu. Mtu Fulani alinielezea kwamba alimuota ndugu yake katika ndoto. Yule ndugu yake aliyekufa akamwambia kwamba mimi niko katika hiki chumba siwezi kulala. Na yule maiti alipokuwa mzima duniani alikuwa hasali. Kwa hiyo ndugu yake alijua hali ya yule maiti wao jinsi alivyo. Na mfano mwingine kuna mwanamke Fulani alikufa baada ya kifo chake watu wakawa wanasema kwamba karogwa. Mmoja wa ndugu yake alimuota ndotoni kama vile yuko katika bustani lenye maua mazuri yenye rangi mbalimbali. Na yule mwanamke alikuwa amekaa kwenye kizingiti cha nyumba na amebadilika kawa msichana mzuri, mara tu yule ndugu yake alipojitokeza mwanamke yule akamsalimia kwa kusema, "Assalaamu Alaykum" kisha akenda zake wala hakumuona. Kwa hivyo ndugu zake walijua hali ya maiti wao.

2. Ni njia moja ya mja kutishwa na kuogopeshwa na Mola wake kwa sababu ya dhambi/madhambi aliyofanya ili ajirekebishe tabiya yake. Mtu Fulani alinielezea kuhusu ndoto aliyoiota ya kutisha usingizini mwake. Mimi nikamwambia kwamba huenda umefanya kitendo kibaya na Mwenyezi Mungu S.W.T. anataka kukuongoza ili usiendelee kufanya kitendo hicho tena. Halafu akasema kwamba ni kweli nimekwisha tambua kosa langu. Na kosa lake lilikuwa kamtolea maneno mabaya mfanyakazi wake wa kike.

3. Ni njia ambayo inatujulisha hali ya watu wanaotuhusu waliohai lakini wako mbali nasi katika hii dunia. Kama alivyotusimulia Mtume S.A.W. kwamba hakika roho hukutana na roho nyingine. Mfano mtu anaishi Oman akamuota ndugu yake ambaye yuko huko Tanzania ambapo hawakuonana naye kwa miaka. Labda huenda akamwambia jambo fulani la siri au akajua hali yake alivyo, mfano mgonjwa.

4. Ni njia ya kusemeshana baina ya maiti na aliyehai. Mfano baba aliyekufa na kuacha deni humwambia mwanawe ndotoni kwamba mimi na deni fulani na ananidai mtu Fulani kwa hiyo tafadhali nilipie hilo deni. Na ajabu kubwa anapouliza hutokea kweli kama alivyoambiwa na baba yake ndotoni.

5. Ni njia ya kumuongoza mja katika haki na kujiepusha na baatil. Mfano mwanamke Fulani alinilielezea kisa ambacho ameota ndotoni kama ifuatavyo: Ameota kama kwamba anaoneshwa Mtume S.A.W. lakini yeye hamuoni. Baadaye kama mtu akamwambia ndotoni kwamba ukitaka kumuona basi lazima uache mambo mabaya unayoyafanya. Baada ya kumhoji ikatokea kweli kwamba yeye anapenda kusikiliza miziki na kufanya mambo ambayo yamekatazwa katika sheria ya dini.

6. Ni njia ya Mola kumuonesha mja katika ndoto amali njema/mbaya anayoifanya.


Asalam Alaikum Waarahmatullahi Wabarakatuhu MIMI NI KIJANA NA




NDOTO YA MSICHANA AMEOTA MCHUMBA WAKE AMEKUJA KUMCHUKUWA KWA GARI.

Msichana Fulani ameota anasema: Mimi nimeota kuwa mchumba wangu aliyekuwa nje ya nchi amekuja kunichukuwa kwa gari yake. Tukavuka daraja kwa gari na pembezoni mwa ile barabara yote ilikuwa imepandwa miti pamoja na miwaridi. Baadaye tukafika katika nyumba fulani ambayo nyumba hiyo ilikuwa na milango miwili. Yeye aliingia katika mlango mkubwa nami niliingia katika mlango mdogo ambao ulikuwa umefungwa kisha nikaufungua. Na nilipoingia ndani niliona pia miti katika bustani ya nyumba halafu nikamuona mchumba wangu ameingia kuoga, alipotoka akaanza kuvaa nguo nzuri kabisa na kuliani kwake msahafu na amefuatwa na kijana mdogo kuliko yeye kwa umri. Baada ya hapo akaniambia, "Haya tutoke nje." Nikatoka pamoja naye. Jee, nini tafsiri yake?


Mfasiri akamwambia: Ndoto yako ni khabari njema kwa ubora wa kuchagua kwako mume mwema. Kisha amejisafisha na madhambi na msahafu kuliani kwake. Ama vazi lake katika nguo nzuri ni wewe. Kwani vazi la mume ni mke wake.


NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA AMEPEWA MAYAI MATATU.

Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi nimeota mjomba wangu amenipa mayai matatu nikayapokea kwa mikono miwili. Jee, nini tafsiri yake?


Mfasiri akamwambia: Ndoto inaashiria kwamba utazaa mabinti watatu baada ya kufunga ndoa.
NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA KATIKA NYUMBA YAO PANYA WENGI PAMOJA NA NYUKI WENGI

Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi nimeota katika nyumba yetu panya wengi wanaingia jikoni kisha wanatoka, halafu wanakwenda chumba kingine. Kisha mimi na mume wangu pamoja na wanangu tukaanza kusafisha nyumba kwa detol, baadaye kama tukatoka nje ya nyumba. Tena niliporejea nikaona nyuki wengi wameingia nyumbani lakini sikuwakuta panya. Na nyuki mmoja akaniuma mguuni. Naomba tafsiri yake.



Mfasiri akamwambia: Nyinyi mlikuwa mna kazi inayowaletea rizki lakini mliipuuza na kuiacha. Mkashika kazi mpya hata hivyo pia inawaleteeni faida. Lakini wewe utapatwa na udhia kutoka kwa watu watakaojiingiza katika shughuli hiyo.

NDOTO YA MTU AMEOTA MENDE WENGI JUU YA PAA LA NYUMBA YAO.
Mtu mmoja ameota anasema: Mimi nimeota ndotoni mende wengi juu ya paa la nyumba yetu. Kisha nikaleta dawa ya kupuliza, nikawapulizia baadaye hakubakia hata mende mmoja juu ya paa ila wote walikimbia na kujificha. Lakini nilimkuta mende mmoja tu yupo juu ya heater la kuchemshia maji.


Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, nyumba yenu ina kitu kinachotokana na hasad, lakini Mola atakiondosha insha-allah.

NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA ANASHAMBULIWA NA PANYA WENGI.
Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi nimeota niko katika nyumba ngeni ambayo sijapata kuiona katika maisha yangu. Mara wakaja panya wengi wenye rangi ya kijivu wakanishambulia wakaanza kuutafuna mkono wangu wa kulia na huku mimi nautikisa na kuuyumbisha. Lakini wapi! Wale panya wameung`anga`nia hawataki kuuachia. Na mimi sikujua nini la kufanya, baadaye nikasoma Ayatul Kursiy kwa sauti kubwa nikaendelea hivyo mpaka wale panya wakaanza kuuachia. Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba mkono wangu ulikuwa unaniuma wakati wale panya wako mkononi, walipokimbia mkono ukarejea kama kawaida wala sikuhisi kitu. Nikawa natafuta hospitali ili niende wakauone ingawa mimi sikuhisi kitu chochote.




Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, kama inavyodhihirika ndoto yako wewe unakesha wakati mwingine, inakuwa usiku wako ni mchana na mchana wako ni usiku. Lakini hutadhurika Inshaa-allah. Na panya kuutafuna mkono wako wa kulia hiyo itaathiri riziki yako. Ni juu yako kwenda mapema kulala hata upate riziki.




NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA ANAZAA SAMAKI WENGI KISHA WAKAGEUKA NYOKA WENGI WADOGO.
Mwanamke mmoja anaelezea ndoto yake anasema: Mimi nimeota nazaa na mzalishaji alikuwa pamoja na mimi ananisaidia wakati wote ule wa kuzaa. Nilikuwa nikihisi maumivu makali sana. Nikazaa samaki wengi baadaye hao samaki wageuka nakuwa nyoka wengi wadogo. Na ilikuwa ikinitoka vipande vya damu wakati wa kuzaa. Kisha nikaamka na ilikuwa wakati huo wa Alfajiri. Jee, nini tafsiri ya ndoto hii.


Mfasiri akamwambia: Kuzaa ni raha, kupata faraji, kulipa madeni na toba. Na samaki ni mali. Wewe unapenda uruzukiwe. Lakini hiyo mali itakayopatikana ni katika njia mbaya. Kwasababu samaki wamegeuka kuwa nyoka. Na mapande ya damu katika ndoto ni mali isiyo ya halali au dhambi. Lakini wewe utakapojua utatubia kwa msaada wa watu. Na maumivu ndotoni ni kujuta kwa dhambi.


5.NDOTO YA MTU AMEOTA NYUMBA YAKE IMEJAA NYOKA WENGI.

Mtu Fulani alimjia Ibn Siyriin akamhadithia ndoto yake akasema: Mimi nimeota nyumba yangu imejaa nyoka wengi.


Akamfasiria akamwambia: Mche-Mungu usiwaweke nyumbani kwako maadui wa Waislamu.

DOTO YA MWANAMKE AMEOTA AMEKWENDA KWA SHOGA YA MAMA YAKE AKAKATWA NYWELE ZAKE.
Mwanamke mmoja ameota anasema: Mimi nimeota ndotoni nimekwenda kwa shoga ya mama yangu, na mahali hapo anapoishi pana sehemu ya kunyolea. Naye ndiye alikuwa kinyozi akanikata nywele zangu. Lakini kusema kweli yeye si kinyozi. Baada ya kunikata mimi sikupendezewa na mkato wa nywele zangu zilivyokatwa. Jee, nini tafsiri yake?


Mfasiri akamwambia: Ndoto inaashiria patatokea ugomvi baina yako na baina ya mtu wa karibu yako kwasababu ya mwanamke fulani anakufanyia ubaya. Na wewe pia unabeba sehemu ya jukumu kwa ugomvi utakaotokea.


NDOTO YA MWANAMKE ALIYEOLEWA AMEOTA ANAAMBIWA NA BABA YAKE, "ATAOLEWA NA MUME WAKE."
Mwanamke Fulani anasema: Dada yangu aliyeolewa ameota ameachwa. Akamjia baba yangu na fustani ya harusi akamwambia, "Leo ni ndoa yako atakuoa mume wako." Akaichukua ile fustani akampa dada yake mkubwa (hajaolewa) akamwambia, "Wewe olewa nayo hii fustani." Akaichukua dada yangu mkubwa ile fustani na alikuwa nacho kikuku (aina ya bangili) cheupe akampa dada yangu mdogo kwa mkufu mwingine kutoka kwa mume wa dada yangu akamwambia, "Hii ni nzuri kuliko aliyonayo mkononi dada yangu mkubwa" Dada yangu mdogo akenda nayo ile fustani na mkufu kwa dada aliyeolewa kusudi ajaribu kumridhisha ili olewe. Akazichukua akenda nazo kwa baba yangu. Nilikuwa mimi na yeye na baba yangu, akazungumza baba yangu kwamba leo ni ndoa yangu mimi na yeye. Nilikuwa nayo fustani nyeupe pia. Baba yangu akasema, "Dada yako ataolewa na mfanyabiashara tajiri na atakuwa mwenye furaha." Akasimama na huku amekasirika kwasababu ya maisha yake. Baba yangu akamwambia, "Usikasirike na ndoa yako hii, ni bora kuliko ya mwanzo." Akamjibu, "Ndoa ya mwanzo ilikuwa jeneza na kuingia nyumba ya mume wangu ni kaburi." Baba yangu akamjibu, "Ndoa yako hii ni afadhali kuliko ndoa iliyopita." Kwahiyo akaridhika. Jee, nini tafsiri yake?



Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, pengine ndoto yake inaashiria posa itakayokubalika kutoka kwa mwanaume mwingine si huyo mtalaka wake. Na huyo mwanaume ni mwenye mali na mwenye tabia nzuri. Na mkufu ni kufunga ndoa na fustani nyeupe ni furaha njema sana.

NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA WATU WANAMWITA BINTI YAKE HURULAENI.

Mwanamke mmoja ameota anasema: Mimi nimeota jina la binti yangu limebadilika, watu wanamwita kwa jina la, "Hurulaeni." Ila mimi tu namwita kwa jina lake. Jee, nini tafsiri yake? Ifahamike kwamba mimi ninaye huyu binti mmoja tu.


Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, pengine binti yako ni mzuri sana wa kupendeza mwenye macho makubwa na yaliyopakwa wanja. Anavutia na macho ya watu yanamuelekea yeye. Kwahiyo ni juu yenu kumwepusha na kijicho cha watu na hasad.
NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA YUPO PAMOJA NA MAKASISI NA WATAWA WA KIKE NDANI YA GARI.
Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi ni Mwanamke Mwislamu ambaye nimeolewa, lakini nimeota niko ndani ya gari tunaelekea kanisani nikiwa pamoja na makasisi (priests) na watawa wa kike (nuns). Na tulipowasili tuliingia wote pamoja kanisani. Jee, nini tafsiri yake?


Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, wewe unahudhuria hafla (sherehe) za harusi zina baadhi ya nyimbo na kucheza ngoma.

NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA YUPO PAMOJA NA MAKASISI NA WATAWA WA KIKE NDANI YA GARI.
Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi ni Mwanamke Mwislamu ambaye nimeolewa, lakini nimeota niko ndani ya gari tunaelekea kanisani nikiwa pamoja na makasisi (priests) na watawa wa kike (nuns). Na tulipowasili tuliingia wote pamoja kanisani. Jee, nini tafsiri yake?


Mfasiri akamwambia: Mwenyezi Mungu anajua, wewe unahudhuria hafla (sherehe) za harusi zina baadhi ya nyimbo na kucheza ngoma.

265.NDOTO YA MWANAMKE ALIYEOLEWA AMEOTWA ANAOLEWA MARA YA PILI.
Mwanamke mmoja ameotwa anasema: Mimi ni mwanamke niliyeolewa na nina watoto wawili wala sifanyi kazi. Dada yangu ameniota naye ni mdogo kwangu kwamba nimevaa fustani (gauni) ya harusi nzuri sana bila ya veli ya harusi. Nami nimekaa katika nyumba ya familia yangu. Na watu na majirani wamekusanyika kama vile sherehe ya harusi, na mume wangu na watoto wangu wamehudhuria pia. Dada yangu alikuwa akishangaa vipi naolewa mara ya pili, nami nimekwisha olewa na mume wangu na watoto wangu wamehudhuria sherehe ya harusi? Naomba tafsiri ya hii ndoto.


Mfasiri akamwambia: Utapata furaha mfano wa furaha ya ndoa, ya kazi nzuri, au mimba au kukubaliwa kusoma Chuo Kikuu.

NDOTO YA MWANAMKE AMEOTA YUPO HOSPITALINI.
Mwanamke mmoja ameota anaelezea anasema: Mimi nimeota niko hospitalini lakini hakunizuru mtu yeyote yule katika jamaa zangu na hata tabibu, na hospitali hiyo inaitwa Sa`ad. Na katika kitanda changu palikuwa na msichana pamoja na jamaa yake akanisalimia kisha akanibusu wakaondoka wote nikabaki peke yangu. Kisha nikajiona nimesimama katika mlango wa ukumbi na katika mkono wangu wa kushoto Qur-ani na karatasi yake ina rangi nyekundu. Lakini maandishi yake ni ya rangi nyeusi. Na mtoto wa kiume wa mama yangu mdogo alikuwa akiisoma halafu akaondoka. Na mimi nikaingia katika ukumbi nikakaa hapo.


Mfasiri akamwambia: Ndoto yako ya hospitali inayoitwa Sa`ad ni dalili kwamba wewe unangojea muradi (jambo/haja inayohitajiwa kupatikana). Wapo wasichana wa jamaa zako waliokaribu wataolewa kabla yako. Lakini hata wewe pia ni karibu. Na kusoma Qur-ani ni dalili ya mtoto wa mama yako mdogo anarejesha amana za watu na ameongoka katika haki. Anaamrisha mema na anakataza maovu kwa kauli ya Mola (...Wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu. Wanamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na wanaamrisha mema na wanakataza maovu...)

NDOTO YA MWANAMKE AMBAYE HAJAOLEWA AMEOTA AMEZAA MTOTO WA KIKE.

Mwanamke mmoja ameota anasema: Mimi ni mwanamke sijaolewa nimeota nimezaa mtoto wa kike. Jee, nini tafsiri yake?




Mfasiri akamwambia: Ndoto ya wewe kuzaa mtoto wa kike ni dunia na mlango wa kheri na furaha.


NDOTO YA MWANAMKE MJAMZITO AMEOTA AMEZAA MTOTO MZURI.
Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi ni mwanamke mjamzito nimeota nimezaa mtoto mweupe mzuri. Jee, nini tafsiri yake?



Mfasiri akamwambia: Ndoto inaashiria kwamba kweli utazaa mtoto mzuri. Lakini jihadhari naye asije akapigwa kijicho.
NDOTO YA MWANAMKE MJAMZITO AMEOTA AMEZAA MTOTO MZURI.

Mwanamke Fulani ameota anasema: Mimi ni mwanamke mjamzito nimeota nimezaa mtoto mweupe mzuri. Jee, nini tafsiri yake?



Mfasiri akamwambia: Ndoto inaashiria kwamba kweli utazaa mtoto mzuri. Lakini jihadhari naye asije akapigwa kijicho.